Monday, December 17, 2012

TIGO NA MAMBO MAPYA


Meneja Mauzo na Usambazaji wa Kampuni ya Tigo Goodluck Charles, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu huduma mpya inayomuwezesha mteja kununua kifurushi cha Extreme kupitia Tigopesa, kushoto ni Afisa Masoko wa Tigo Jacqeline Nnunduma na Afisa Uhusiano wa Tigo Mariam Mlangwa.
Afisa Masoko wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Tigo Jacqueline Nnunduma akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wakitangaza huduma mpya ya kununua kifurushi cha Xtreme kupitia Tigopesa.
FAIDA atakazopata mteja atakayetumia huduma ya Xtreme kupitia tigopesa ni pamoja na muda wa nyongeza wa Tsh.450 utakao muwezesha kupiga simu kwenda mitandao yote nchini. Mbali na hilo wateja wataweza kununua vifurushi hivyo kwaajili ya ndugu jamaa na marafiki.

No comments:

Post a Comment