Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali Katibu wa Mufti Mkuu wa
Zanzibar, Sheikh Fadhili Soraga ambaye amelazwa katika chumba cha
dharura katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kufuatia majeraha ya
usoni na kifuani yaliyotokana na kumwagiwa tindikali na watu
wasiojulikana wakati akifanya mazoezi katika Uwanja wa Mwanakwerekwe
mjini Unguja jana. Rais ambaye amerejea leo Jumanne Novemba 6, 2012
akitokea katika ziara ya kikazi ya juma moja katika mikoa ya
Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Singida, amemtakia Sheikh Soraga nafuu
ya haraka. Picha na Ikulu
No comments:
Post a Comment