ADVERTISEMENTS/MATANGAZO
Thursday, May 31, 2012
SUALA LA AFYA YA UZAZI SALAMA LIPEWE KIPAUMBELE MCHAKATO WA KATIBA
Mkurugenzi wa Chama cha Wanasheria wanawake TAWLA Mwanasheria Tike Mwampipile akizungumza na washiriki wa semina ya mapendekezo ya
kuwepo kwa sheria ya Afya ya Uzazi Salama katika
mchakato wa maoni ya kuandikwa kwa Katiba Mpya iliyomalizika jana
kwenye ukubi wa hoteli ya Blue Pear Ubungo Plaza jijini Dar es salaam.
BAADHI YA WAREMBO WATAKAOPANDA JUKWAANI KATIKA SHINDANO LA MISS NYAMAGANA JIJI MWANZA LEO
| Amina. |
| Brenda |
MKUTANO WA SHIRIKISHI LA NGUMI LA DUNIA IBF WAENDELEA HUKO HONOLULU MAREKANI
Rais wa IBF/USBA duniani Daryl Peoples wa Marekani kushoto akiwa
amesimama na Rais wa IBF bara la Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya
Uajemi Mtanzania Onesmo Ngowi siku ya ufunguzi wa mkutano huo tarehe 31
May, 2012.
Rais Peoplers aliwakaribisha wajumbe na kuwasomea taarifa ya mwaka
ya IBF/USBA ambapo zaidi ya mapambano ya ubingwa 349 yalifanyika chini
ya IBF/USBA mwaka jana.
Mkutano huo ulihutubiwa pia na Rais wa IBF katika bara la Afrika,
Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi Mtanzania Onesmo Ngowi. Aidha
mwakilishi wa IBF katika bara la Ulaya Roberto Reya wa Italia naye
alihutubia mkutano huo.
Katika mkutano huo taarifa ya kifo cha bondia wa Thailkand
Thangthong Kiattaweesuk aliyekuwa na miaka 35 kilitolewa rasmi. Bondia
Kiattaweesuk alikufa katika ajali ya gari akiwa na mkewe, mtoto mmoja na
ndugu yake baada tu ya kushinda pambano lililompa nafasi ya kupigana na
bingwa wa IBF wa dunia katika uzito wa Feather Geoffrey Mathebula wa
Afrika ya Kusini.
Kiattaweesuk alimpiga bondia wa Kenya Geofrey Munica kwa KO raundi ya 10 katika pambano la kugommbea mkanda wa mabara wa IBF.
Pamoja na ufunguzi huo leo kutakuwa na semina ya utibabu pamoja na semina ya majaji. Mkutano huo utamalizika tarehe 2 Juni.
Mkutano huu unahudhuriwa na wajumbe 6000 toka nchi 204 duniani
kote. Ujumbe wa Afrika ni moja ya ujumbe unaoshiriki katika mkutano huu
maalum wa kuafiki programu ya Utalii wa Michezo itakatowakilishwa na
Rais wa IBF katika bara la Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi
Mtanzania Onesmo Ngowi.
TAIFA STARS YAWASILI ABDIJAN,KIM ASEMA MECHI ITAKUWA NGUMU
Kikosi
cha Taifa Stars kimewasili hapa Abidjan (Mei 31 mwaka huu) mchana huku
Kocha Mkuu wa timu hiyo Kim Poulsen akisema mechi dhidi ya Ivory Coast
itakuwa ngumu.
Stars
yenye wachezaji 21 ilikuwa iwasili hapa asubuhi, lakini ndege
iliyobadilisha Nairobi ilichelewa kuondoka kwa saa tatu. Mechi ya mchujo
ya Kombe la Dunia kati ya Taifa Stars na wenyeji Ivory Coast (Tembo)
itachezwa Juni 2 mwaka huu Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny kuanzia saa
11 kamili jioni ambapo Tanzania itakuwa saa 2 kamili usiku.
Licha
ya kwanza, Stars ililazimika kuacha wachezaji wawili dakika za mwisho
(Haruna Moshi na Nassoro Cholo), Kim amesema kikosi chake ambacho
kimefikia hoteli ya Ibis bado kimejipanga vizuri kwa ajili ya mechi
hiyo.
“Tunaiheshimu
Ivory Coast kwa vile ni timu ambayo inaundwa na baadhi ya wachezaji
nyota wa dunia kama akina Drogba (Didier) na Yaya (Toure), lakini
wajiandaa kupata wakati mgumu kutoka kwetu,” amesema Kim ambayo kikosi
chake baada ya kuwasili hapa kilipata fursa ya kufanya mazoezi jioni.
Kikosi
cha Stars kinaongozwa na nahodha wake Juma Kaseja akisaidiwa na Aggrey
Morris. Wachezaji wengine waliopo hapa na kikosi hicho ni Mwadini Ally,
Deogratius Munishi, Amir Maftah, Erasto Nyoni, Kelvin Yondani, Waziri
Salum, Shomari Kapombe na Juma Nyoso.
Jonas
Mkude, Mwinyi Kazimoto, Salum Abubakar, Shabani Nditi, Edward
Christopher, Mrisho Ngasa, Frank Domayo, Mbwana Samata, Ramadhan
Singano, Simon Msuva na John Bocco.
Mbali
ya Kim, Benchi la Ufundi lina Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi), Juma
Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Mukebezi (Meneja wa timu), Juma
Mwankemwa (Daktari wa timu), Frank Mhonda (Physiotherapist) na Alfred
Chimela (Mtunza vifaa).
Msafara
wa Stars hapa unaongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Crescentius Magori lakini pia yupo
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Dioniz Malinzi ambaye amekuja kushuhudia mechi hiyo.
MISS MTWARA KUFANYIKA JUMAMOSI JUNI 2 MJINI MTWARA
| Warembo watakaopanda jukwani kumtafuta Miss Mtwara 2012 Wakimsikiliza mkufunzi wao Isabela mpada (MISS RUVUMA 2006) siku ya jumamosi Juni2 katika ukumbi wa makonde beach |
Warembo watakaopanda jukwani kumtafuta Miss Mtwara 2012 Wakimsikiliza
mkufunzi wao Isabela mpada (MISS RUVUMA 2006),Pamoja na muandaaji wa
shindano Rajab Mchatta. siku ya jumamosi Juni 2 katika ukumbi wa
makonde beach
NMB YAZINDUA PROMOSHENI YA JENGA MAISHA YAKO NA NMB
Kwa kutambua kuwa watanzania wengi wanaweka akiba ili kutimiza malengo
mbalimbali katika maisha,leo benki ya NMB imezindua promosheni
iitwayo jenga maisha yako na NMB itakayomwezesha mteja wake kuingia
kwenye droo na kushinda tani ya saruji, mabati ya kuwezeka,
amana maradufu, ada za shule, fulana za NMB pamoja na mabegi ya shule.
Akizungumza wakati wa
uzinduzi wa promosheni ya JENGA MAISHA YAKO NA NMB, Mkuu wa idara
ya Masoko na Mawasiliano Bw. Imani Kajula kushoto katika picha amesema “wateja wengi wanaweka amana ili kutimiza malengo
mbalimbali na ndio maana, benki ya NMB imezindua promosheni ya JENGA
MAISHA YAKO NA NMB itakayowezesha wateja wote wa NMB Bonus Account na
NMB Junior Account watakaofungua akaunti au kuongeza amana kwenye akaunti
zao za NMB Bonus Account au NMB Junior Account kupata riba ya kuvutia
hadi asilimia 10 kutegemeana na kiwango cha amana kilichowekwa” .
Kupitia droo ambazo
zitachezeshwa kila mwisho wa mwezi kwa muda wa miezi mitatu kuanzia
leo, sio tu zitawaongezea watanzania tabia ya kujiwekea akiba lakini
pia itasaidia watakaoshinda kufikia malengo waliyojiwekea..
Fungua NMB Bonus Account
au NMB Junior Account leo na ushinde!!!
WAZAZI WAPINGA WATOTO WAO WANAOSOMA SHULE ZA MSINGI KISING'A KUFANYISHWA KAZI MDA WA MASOMO
Wanafunzi wa shule ya msingi Kising'a Isimani wilaya ya Iringa
vijijini wakiwa wamebeba ndoo za maji kwa ajili ya ujenzi wa
nyumba ya mwalimu jana majira ya saa 9.45 asubuhi muda ambao
walipaswa kuwepo darasani kama walivyokutwa na mpiga picha wetu. TABIA ya
uongozi wa shule ya msingi Kising'a Isimani wilaya ya Iringa
kuwatumikisha kazi wanafunzi asubuhi wakati wa vipindi vya masomo
imepingwa vikali na baadhi ya wazazi wanaosomesha watoto wao
katika shule hiyo na kuiomba wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi
kuingilia kati suala
hilo.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi leo kijijini hapo wazazi hao walisema kuwa uongozi wa shule hiyo ya msingi Kising'a kila siku kabla ya watoto kuingia madarasani wamekuwa wakiwatuma katika kazi mbali mbali ikiwemo ya kuchota maji kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mwalimu.
Alisema Jonh Kalinga kuwa tayari wamepata kuulalamikia uongozi wa shule hiyo na kuukanya kacha kuwatumikisha watoto hao majira ya masomo ila bado vitendo hivyo vya wanafunzi kukatishwa vipindi na kwenda kufanya kazi za walimu vimekuwa vikiendelea.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi leo kijijini hapo wazazi hao walisema kuwa uongozi wa shule hiyo ya msingi Kising'a kila siku kabla ya watoto kuingia madarasani wamekuwa wakiwatuma katika kazi mbali mbali ikiwemo ya kuchota maji kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mwalimu.
Alisema Jonh Kalinga kuwa tayari wamepata kuulalamikia uongozi wa shule hiyo na kuukanya kacha kuwatumikisha watoto hao majira ya masomo ila bado vitendo hivyo vya wanafunzi kukatishwa vipindi na kwenda kufanya kazi za walimu vimekuwa vikiendelea.
RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA WANANCHI JUU YA VURUGU ZILIZOTOKEA HIVI KARIBUNI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohd
Shein akizungumza na Wanahabari wa Vyombo mbalimbali vya Habari Nchini
kuhusiana na Vurugu Zilizotokezea Zanzibar,hapo katika ukumbi wa Ikulu
Mjini Zanzibar.Ukiwa ni Utaratibu wake wa kuzungumza na Vyombo vya
Habari kila ifikapo mwisho wa Mwezi.
Na Juma Mohammed,MAELEZO Zanzibar
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed
Shein amesema kwamba Serikali italinda amani kwa nguvu zote na kuonya
kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua watakaochochea na kufanya
vurugu.
Akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari Ikulu Zanzibar jana,Dk. Shein
alisema “Tutailinda amani kwa nguvu zote,atakayethubutu kuchezea
tutamshughulikia kwa mujibu wa sheria”
Rais
Shein alisema amesikitishwa sana na vitendo vilivyotokea wiki iliyopita
na kuelezea vurugu hizo zimeharibu sifa njema ya Zanzibar ambayo kwa
miaka mingi ianjulikana kwa uvumilivu wa kidini kiasi cha hata Serikali
ya kikoloni mwaka 1953 kuamua kufanya shindano la uchoraji wa stamp ya
uvumilivu wa kidini.
“Kwa
masikitiko makubwa nataka kusema kuwa vitendo vilivyotokea vya kuvunja
amani ni vya aibu, vimetusononesha sana na haya wananchi lazima wajue
kuwa amani yetu ni muhimu kuliko jambo lolote lile” Alisema Rais Dk. Shein.
RAIS KIKWETE AFUNGUA MKUTANO WA AFDB MJINI ARUSHA LEO
![]() |
| Rais wa benki ya maendeleo ya Afrika (AFDB) Dr.Donald kaberuka akihutubia wakati wa sherehe za ufunguzi wa mkutano wa 47 wa mwaka wa benki ya maendeleo ya Afrika (AFDB) Mjini Arusha. |
![]() |
| Rais wa jamhuri ya Ivory Cost Dr Alassane Ouattara akihutubia wakati wa sherehe za ufunguzi wa mkutano wa 47 wa mwaka wa benki ya maendeleo ya Afrika (AFDB) Mjini Arusha. |
WAZIRI MKUU KUMWAKILISHA RAIS KIKWETE NCHIN ANGORA
![]() |
WAZIRI MKUU Mizengo
Pinda
WAZIRI MKUU Mizengo
Pinda anaondoka Dar es Salaam leo mchana (Alhamisi,
Mei 31, 2012) kwenda Luanda, Angola kuhudhuria
kikao cha Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika
(SADC).
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Waziri Mkuu Pinda anahudhuria
mkutano huo kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete ambaye leo anatarajiwa kufungua
mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) huko Arusha.
Mara baada ya kuwasili, leo jioni Waziri Mkuu atahudhuria kikao cha
TROIKA ambacho kinajumuisha Wakuu wa Nchi kitakachofanyika Ikulu ya nchi hiyo
na usiku atashiriki hafla maalum iliyoandaliwa kwa viongozi wakuu wa nchi za
SADC.
Mkutano huo wa Wakuu wa Nchi za SADC ambao
umepangwa kufanyika kesho (Juni Mosi, 2012), utatanguliwa na mkutano wa
mawaziri unaoanza leo (Alhamisi, Mei 31, 2012) chini ya uenyekiti wa Waziri ya
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe.
Waziri Mkuu anatarajiwa kurejea jijini
nchini kesho kutwa (Jumamosi, Juni 2, 2012).
MAKAMU WA RAIS DKT BILAL ASAINIANA MKATABA NA MAKAMU WA RAIS WA KWANZA WA IRAN.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, na Makamu wa Rais wa Kwanza wa Iran, Mhe. Mohammad
Reza Rahimi, wakisainiana mkataba wa makubaliano ya pamoja ya masuala
mbalimbali yanayohusu uhusiano wa nchi hizo mbili, wakati wa hafla hiyo fupi iliyofanyika kwenye
Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam jana Mei 30, 2012
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, na Makamu wa Rais wa Kwanza wa Iran, Mhe. Mohammad
Reza Rahimi, wakibadilishana mkataba baada ya kusainiana mkataba huo wa makubaliano
ya pamoja ya masuala mbalimbali yanayohusu uhusiano wa nchi hizo mbili, wakati wa hafla hiyo fupi iliyofanyika kwenye
Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam jana Mei 30, 2012
DROO YA TANO YA PROMOSHENI YA VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO NA SBL,YANGURUMA TENA,MWANZA WAENDELEA KUVUNA ZAWADI
ZUKU YAFANYA HAFLA YA KUTANGAZA UDHAMINI WA TAMASHA LA ZIFF
![]() |
| Mmoja wa wasanii wa kundi la Shilole akitumbuiza mbele ya wageni mbalimbali waliohudhuria katika hafla hiyoi. jana jion |
![]() |
| Waigizaji wa filamu mbalimbali wakiwa wamesimama mbele wakati walipokuwa wakitambulishwa katika hafla hiyo na mwenyekiti wa ZIFF Bw. Mahmoud Thabit Kombo. |
![]() |
| Kutoka kulia ni Jacob Steven. Raymond Kigosi na Cloud waigizaji wa filamu za Bongomovie wakiwa katika hafla hiyo |
![]() |
| Mwigizaji Aunt Ezekiel kushoto akiwa na waigizaji wenzake. |
![]() |
| Mwigizaji Jaquiline Walper kushoto akiwa na waigizaji wengine katika hafla hiyo wa tatu kutoka kulia ni mchezaji wa timu ya Simba Uhuru Selemani. |
Subscribe to:
Comments (Atom)





















