Wakati klabu ya Simba ikiwa
imejihakikishia kukamilisha usajili wa kinda la Azam under 20, Ibrahimu
Jeba ambaye leo hii asubuhi alionekana kwenye mazoezi ya gym ya Simba -
maeneo ya Chang'ombe. Uongozi wa klabu ya Azam FC umesema Simba
inajidanganya kuhusu kumsajili mchezaji huyo ambaye Azam walimpeleka
Villa Squad kwa mkopo kwa kujifua zaidi msimu uliopita.
Meneja wa klabu ya Azam FC, Patrick
Kahemele amesema mabingwa wa Tanzania bara wanafanya uhuni kwenye
uhamisho wa mchezaji huyo ambaye bado ana mkataba na klabu hiyo
inayomilikiwa na mfanyabiashara Salim Bakheresa. "Simba wanafanya uhuni
katika hili kama ilivyo kawaida yao, Jeba ni mchezaji wetu halali na
bado ana mkataba na Azam. Kumbukumbu sahihi nilizonazo ni kwamba
Ibrahimu Jeba alisaini mkataba wa kuichezea Azam kwa miaka miwili mwezi
Desemba 2011 na akachukua kiasi cha fedha kama ada ya usajili - kabla ya
kuelekezwa kwamba akacheze Villa Squad kwa mkopo ili apate nafasi ya
kujifua then msimu huu arudi Azam FC. Simba wakaenda wakamrubuni
asicheze Villa, na Jeba bado mdogo hivyo ikawa rahisi kumrubuni, na Azam
hatukutaka kufanya nao malumbano kwa sababu suala hilo tayari tuna
mkataba ambao umesajiliwa kabisa na TFF, ambao walishatuambia haki zetu
za msingi zitalindwa."
Kahemele alipoulizwa ikiwa Simba
wanataka kulimaliza hilo suala itabidi walipe kiasi gani alijibu,
"Kiukweli sie tulishatangaza mapema kwamba hakuna mchezaji yoyote ambaye
ameachwa wala yupo sokoni kwa msimu ujao. Hivyo kama Simba wanamtaka
Ibrahimu Jeba kihalali basi atawagharimu sana kwa kuwa sisi tunamuona
Jeba akiwa na thamani ya Shilingi millioni 50 na uwachanganye wachezaji
wawili wa Simba Jonas Mkude na Shomari Kapombe, then hapo tunaweza
kuwafikiria kuwaachia Jeba vinginevyo haitowezekana Jeba kuichezea klabu
yao."
No comments:
Post a Comment